Showing posts with label makala. Show all posts
Showing posts with label makala. Show all posts

Monday 2 November 2015

Motorola Launches DROID Turbo 2 And It Just Won’t Break


motorola-unbreakable-phone-1
It doesn’t matter how advanced or smart your smartphone is if it gets shattered each time it falls! The flaw isn’t fixated to Apple iPhones, which if you remember would bend inside your pockets, but to almost all the phones (except vintage Nokia) that would easily break.
Motorola has, however, come up with its own hulk version of a smartphone that just won’t break. Motorola DROID Turbo 2 is the phone which won’t bother you with the unnecessary care-taking measures while using. The DROID Turbo 2 runs on the USP of a shatterproof display along with several upgrades and is a strong contender for the people’s choice.The Turbo2 display has a five-layered structure that absorb shocks keeping your smartphone’s screen intact, claims Motorola. Also, the display is little elastic rather than being rigid to incorporate up to a certain amount force.
The Motorola DROID Turnbo 2 has a 5.4-inch Quad HD (2560 x 1440) display which comes with a four-year warranty against shattering and cracking.
After Motorola showcased its phone’s sturdiness against iPhone in an advertisement, the skeptics at CNN performed some of their own tests to check the claims of the perfect phone for the imperfect people.
Watch the official “shatterproof display” ad for DROID Turbo 2 by Motorola.

Also, watch the experiment by CNN.

+

Sunday 28 December 2014

MWAKA 2014 UNAISHIA NA HUJAFANYA CHA MAANA, WHY? KWA NINI?

Nianze kwa kumshukuru Mungu kwa upendo aliouonesha kwangu na kuniwezesha kuiona siku ya leo nikiwa mzima. Nadiriki kushukuru kwa sababu, wapo waliotamani kuiona wiki hii wakiwa wazima lakini baadhi wameshaondoka kwenye ardhi hii huku wengine wakiwa hoi mahospitalini na majumbani. Ndugu zangu, mwaka ndiyo huo unakaribia kuisha. Najua wapo wanaoumaliza wakiwa wamefanya mambo makubwa lakini pia wapo ambao mioyo yao imesinyaa kwa kuwa, waliyopanga kuyafanikisha hayakutimia.
Mimi nataka kuwatia moyo wale ambao mwaka unaisha bila kufikia mafanikio waliyotarajia. Kumbuka kila jambo linapangwa na Mungu, yawezekana yeye kwa sababu anazojua kapanga ufanikiwe mwaka ujao na siyo huu.
Kikubwa ni kuamini kuwa hakuna linaloshindikana kwako. Wewe ni bilionea mtarajiwa! Wewe ni mmiliki wa makampuni makubwa mtarajiwa nk. Hizo ziwe ni kati ya ndoto zako kubwa kwenye maisha yako ya kesho na huna sababu ya kufa moyo.
Ukifuatilia historia za watu wenye mafanikio makubwa duniani utagundua miaka na miaka ilikatika wao wakiishi maisha magumu lakini hawakunyanyua mikono juu na kusema wameshindwa!Kadiri walivyokuwa wakikumbana na changamoto ndivyo walivyozidi kupambana wakiamini walikuwa wakiyakaribia mafanikio.
Kwa jitihada walizoonyesha kuna wakati Mungu akaamua kuwabandika mikono ya baraka na wakafanikiwa. Wewe pia amini mwaka ujao ni wako wa mafanikio, ongeza bidii.
Hata hivyo, yapo mambo ya msingi ya kuyazingatia ili mwaka ujao ujiweke kwenye nafasi nzuri ya kuingia kwenye historia ya watu waliofanikiwa.
Ni vyema ukajipanga upya
Waswahili wanasema, kuteleza si kuanguka, kama ulishindwa kufanikiwa mwaka huu, kaa chini tena na uorodheshe malengo yako. Unashauriwa kutafakari upya na kutafuta njia sahihi za kuweza kufanikisha malengo hayo.
Thubutu tena na tena
Maisha siku zote ni mapambano. Maisha ni kutoogopa kujaribu kwa kuhofia kushindwa.  Kamwe usiogope kuthubutu tena na tena kwani hata ukishindwa itakuwa ni hatua ya kuelekea kwenye mafanikio.
Dadisi, ongea na waliofanikiwa
Kuwa tayari kujifunza kutoka kwa wengine ambao wamemaliza mwaka huu wakiwa wamefanikiwa katika mambo yao. Jaribu kudadisi na kung’amua ni kwa namna gani wameweza kufikia malengo yao ili na wewe ujifunze kitu kutoka kwao.
Kukata tamaa ni mwiko
Katika kujaribu kufikia malengo yako ni wazi umekutana na vikwazo vya hapa na pale na wakati mwingine kuhisi huwezi kuendelea tena.
Siku zote vikwazo unavyokutana navyo viwe ni changamoto kwako ya kujipanga upya na kuanzisha tena mapambano ya kufikia malengo yako.
Kukata tamaa ni mwiko kwani inaelezwa kuwa, idadi kubwa ya watu wanaoishi maisha yasiyokuwa na nyuma wala mbele wameathiriwa na tabia ya kukata tamaa.
Omba ushauri
Katika mbio za kufikia malengo yako, usiishi kama kisiwa, wakati mwingine omba ushauri wa kimawazo pale utakapokwama.  Usikubali kubaki na msongo wa mawazo, jaribu kutafuta msaada na ushauri kwa watu unaowaamini.
Anasa ni sumu
Matumizi mabaya ya fedha na kupoteza muda mwingi katika mambo ya anasa kamwe haviwezi kukusaidia kutimiza ndoto zako.  Daima kazi kwanza, starehe baadaye, ishi kama mtumwa leo, ili utimize ndoto ya kuishi kama mfalme kesho!
Jifanyie tathimini
Katika hatua nyingine ni vyema pia ukachukua muda wako kujitathimini kwa kudadisi sababu ambazo huenda zimekufanya usifanikiwe mwaka huu. Je, matumizi yako ya fedha yalikuwa mabaya kiasi cha kutokuwa makini na kila shilingi uliyokuwa ukiipata? Je, hukujituma sana na hukutumia akili na maarifa yako katika kiwango cha juu?
Je, ulitengeneza mazingira ya kuwapa mwanya maadui wakukatishe tamaa na kukufanya uhisi huwezi? Fanyia kazi maswali hayo!
+

Wednesday 17 December 2014

JINSI YA KUONDOA MADOA YA CHUNUSI

JUISI YA LIMAO NA MAJI YA ROSE
Chukua maji ya rose kiasi kama ni kijiko kimoja na maji ya limao nayo yawe kijiko kimoja paka eneo liloathiriwa na madoa, kaa kwa muda wa nusu saa mpaka saa moja kisha osha uso wako, fanya hivyo kwa muda wa wiki tatu utapona madoa doa yote usoni.
Juisi ya limao na liwa
Chukua juisi ya limao kiasi changanya na liwa kisha paka eneo lililoathirika, kaa kwa muda wa dakika tano utaona matokeo.
Juisi ya limao na unga wa mdalasini pia ni tiba nzuri ya kusafisha uso kuondokana na madoa yote.
Asali na mdalasini
Chukua vijiko vitatu vya asali na kimoja cha mdalasini changanya kisha paka usoni pia ni tiba nzuri inasaidia kwa kiasi kikubwa.
Apple na asali
Chukua apple liponde changanya na asali kiasi, kisha paka usoni mbali na kutibu madoa pia inatibu chunusi.
Maji ya kitunguu swaumu
chukua maji ya kitunguu swaumu paka kwenye madoa yote utaona matokeo.
Nyanya
chukua kipande cha nyanya paka usoni kisha kaa kwa muda wa saa moja nayo ni tiba nzuri.

Tango
Tango pia ni tiba, chukua kipande sugua uso wako kila siku asubuhi utaona matokeo.
Papai
Chukua papai liponde kisha paka usoni litakusaidia kuondoa tatizo la madoa yote usoni.
+

UNATAKA KUPATA UTAJIRI WA HARAKA? SOMA HAPA

HAISHANGAZI kama ukilala maskini ukaamka tajiri. Swali ni je, utaufanyia nini utajiri huo? Amini usiamini inawezekana. Kumbuka, sijasema itakuwa rahisi, nilichokisema ni kwamba inawezekana. Hapa nakuletea dondoo za namna ya kupata utajiri haraka kwa lugha ya mtaani fastafasta.
WEKEZA
Anza kuwekeza ukiwa mdogo yaani kiumri na kidogo ulichonacho. Inawezekana ukaanza hata ukiwa shule ya msingi au hata kama ni shule ya awali sawa tu. Kinachohitajika ni mazingira rafiki ya ujasiriamali. Nakuhakikishia kuwa fedha zako zitaongezeka kila kukicha ukizingatia mambo mengine nitakayoeleza baadaye.
Ni kama mayai yanayotagwa na ndege ambayo baadaye huatamiwa na kuzalisha ndege wengine.
Angalizo; kama unafuatilia makala haya wakati umri umekutupa mkono na hukuweza kuanzia shule za awali lakini una watoto, unaweza kuwatumia kwa kuwatengenezea mazingira ninayoyaeleza. Uwe mwalimu wa ujasiriamali kwa watoto wako au hata wajukuu zako.
Hata kama umri umekwenda lakini Mungu kakujalia kibarua, jaribu kuwekeza asilimia 50% ya mshahara wako katika kujitoa kwa kiwango cha hali ya juu kabisa kutokana na mfumuko wa bei katika soko huru na ugumu wa maisha.
Una uwezekano wa asilimia 50 kwa 50 kutengeneza utajiri au kuanguka ndani ya siku 90.

OA AU OLEWA NA MTU TAJIRI
Najua hapa utakuwa na maswali mengi kwamba nisipooa au kuolewa na mtu tajiri basi nitakufa masikini. Inawezekana pia japo ni kwa asilimia ndogo! Twende mbele zaidi, yaani usemi huu unamaanisha uwe na mwenza wa maisha mwenye maono. Yawezekana msiwe na utajiri kwa maana ya fedha lakini mkawa matajiri wa mawazo ya kijasiriamali. Pale mmoja anapofikia ukomo wa mawazo na kuhisi kushindwa, basi mwenza wake awe nguzo ya kushauri na siyo kukatisha tamaa kabisa kuwa sasa tumeshindwa! Hapana, muote ndoto tofauti lakini mshirikiane kuzitafsiri ili kufikia mafanikio.

SHINDA BINGO
Hii haimaanisha kuwa utajiri unatokana na michezo ya kubahatisha pekee lakini pia inawezekana ila ni kwa asilimia ndogo. Kumbuka wapo waliozaliwa na bahati zao wakashinda michezo ya kubahatisha wakawa matajiri, mifano ipo. Falsafa ni kwamba ujijengee tabia ya kujaribu kufanya vitu. Hapa narudi kipengele cha kwanza yaani kuwekeza hata katika kitu ambacho huna hakika kama utafanikiwa.
Wajasiriamali wanasema ‘ku-take risk’. Haitashangaza kuona unafanikiwa ghafla na wasiamini katika kujaribu wakaishia kusema unatumia ndumba.
WAZAZI MATAJIRI
Kama umezaliwa katika familia tajiri, ukawa na maono katika ujasiriamali, wewe upo nusu ya safari ya mafanikio. Unachotakiwa kufanya ni kuwa mtiifu kwa kupita kwenye nyayo za baba na mama ukiwashawishi kwa kuwa mwangalifu katika matumizi ya kile wanachokupatia. Usitumie kwa kutupatupa ili wakitangulia mbele ya haki ubaki kuwa vizuri tofauti na inavyotokea kwa baadhi ya familia. Jenga nao ushirikiano wa hali ya juu na wakati mwingine wape mawazo hata kama watayaona ni ya kitoto lakini utakuwa umejijengea mazingira ya wao kukuona sehemu ya utajiri wao.

NENDA SHULE UPATE UJUZI
Elimu ni mtaji mkubwa kuliko hata fedha. Jitahidi kusoma katika mazingira yoyote bila kujali wingi wa miaka utakayopoteza darasani. Jaribu kupata weledi na ujuzi wa kila namna halafu chagua kimoja ambacho kitakupa fedha nyingi.
Itaendelea wiki ijayo.
+

Monday 15 December 2014

ACHA KULA UJANA, PAMBANA SASA KUSAKA MAFANIKIO!

Niwakumbushe tu kwamba, licha ya sarakasi zote tunazofanya kwenye maisha yetu ya kila siku, ni vyema tukamtanguliza Mungu na kufanya yale ambayo ametuamrisha na kuachana na aliyotukataza. Kwa kufanya hivyo atatubariki na mambo yetu yatatunyookea.
Baada ya kusema hayo, sasa nirudi kwenye mada yangu ya wiki hii. Mpenzi msomaji wangu, ukweli ni kwamba kila mmoja wetu angependa kuwa na maisha mazuri au kifupi kwamba awe na fedha nyingi, kwa maana ya tajiri.
Hii ndiyo sababu mara kadhaa umepata kusikia juu ya watu wanaosaka utajiri kwa njia mbalimbali, zikiwemo haramu na ushirikina.
Katika dhana ya kusaka mafanikio, kama lengo la kila mmoja ni kutafuta kazi za ndoto zake au kuanzisha kampuni mpya, vijana wengi wanaweza kuweka malengo yao na kufanikiwa haraka kama wataamua.
Wapo watu wengi waliofanikiwa kushika kiasi cha shilingi milioni moja ya kwanza maishani mwao wakiwa na umri chini ya miaka 30 na hapo ndipo mawazo ya wao kuwa mamilionea yalipochipukia. Hakuna uchawi wowote waliowahi kuufanya ili kuwafikisha walipo sasa.
Nafahamu kwamba inawezekana kuwa na maisha mazuri mapema katika maisha yako kama kweli umedhamiria na ukaamua kupigana.
Kama mfanyakazi kijana, watu wengi watauona umri wako kama tatizo kubwa la kufikia malengo yako. Lakini ukweli ni kwamba ujana wako unaweza kuwa na msaada mkubwa sana kwako.
Wengi niliowahi kufanya nao kazi na biashara walikuwa ni watu wazima, wakati mwingine walikuwa wakubwa kuliko mimi.
Hawa wote walikuwa wanataka kufikia malengo yao lakini baadhi hawakujua ni kwa jinsi gani wangeweza kufika huko wanakofikiri.
Walihitaji kutokea kwa mtu mwenye dhamira na nia anayeifahamu vyema biashara wanayotaka kuifanya.
Hata hivyo, bado kuna hasara pia kwa kuwa kijana na mtu asiye na uzoefu katika kazi au ujasiriamali, lakini unapoamua kukubali umri wako na kuazimia kupigana kuelekea mafanikio, lazima uwaambie watu unaotaka kushirikiana nao kuwa wewe kweli ni kijana, lakini hilo halimaanishi kwamba huelewi unachokifanya, unajua na umedhamiria kuwa bora katika uwanja unaoingia.
Unapobaini kipaji chako, ni lazima ujitoe kukitumia ili kiweze kukupa maisha unayotamani. Na katika hili, usiwe mtu wa kuwa peke yako kimawazo, jaribu kushirikiana na unaowaamini katika mawazo yako, kwamba unafikiri kuhusu kufanya hivi na vile, wasikilize wanavyokushauri, lakini mwisho wa siku ni lazima uamue kwa faida yako mwenyewe.
Nina uhakika yupo mtu sahihi, bila kujali umri wake ambaye mara nyingi hutokea kuwa mkubwa kuliko wewe, atakayekubaliana na mawazo yako na kuamua kuungana na wewe katika kuyafanyia kazi.
Niseme tu kwamba, wewe kijana huu ndiyo muda wako wa kupambana na kusaka mafanikio kwa nguvu zote.
Waliocheza enzi za ujana wao, sasa wanakiona cha mtemakuni. Acha kula ujana, tengeneza maisha yako ya baadaye sasa!
+

Saturday 13 December 2014

ISHU SI KUOA, ILA UNAMUOA NANI KWA VIGEZO GANI?-2

Na Michael Shuma:
Kwa moyo mkunjufu nikukaribishe mpenzi msomaji wa safu hii ya Love and Story, tunapata kujifunza mambo mbalimbali yahusuyo maisha ya uhusiano.
Kwa wale tulioianza mada ya ishu siyo kuoa, ila unamuoa nani kwa vigezo gani wiki iliyopita, hakika wataungana nami kwamba ili uishi usije kujutia ndoa yako, yakupasa kuchagua mke au mume sahihi.
Tunaimalizia mada hii ambapo hakika itakuwa ni funzo kwa pande zote mbili, mwanaume na mwanamke.
Kwenye ndoa kuna wakati wa maradhi. Yawezekana ukaumwa wewe au akaumwa hata ndugu yako, je mkeo atakuwa tayari kukuhudumia. Mbaya zaidi ugonjwa wenyewe unaweza kuwa wa kutia kinyaa, atakuwa tayari kukuhudumia au kuwahudumia ndugu zako?
Lazima ujue kwamba anaweza kustahimili katika hali kama hiyo au maneno yale ya kwamba; “mtaishi kwa shida na raha” yeye atayageuza na kuwa tayari kwa maisha ya raha tu, ya shida hayawezi.
Asiwe mtu wa kwenda na wakati asiyetaka hata kucha zake zisiingie maji kwa kuosha vyombo. Hajui kufua nguo.
Asije kuwa yule wa kufanyiwa kila kitu na dada wa kazi. Yeye ni mtu wa kuelekeza kila kitu halafu dada afanye, suala la kupika kwake ni kizungumkuti.
Mwanamke wa aina hiyo hafai kuwa mama wa watoto. Unafikiri atawafundisha nini wanaye? Ujinga tu!
Mke ndiyo msiri wako, ndiye ambaye anaweza kukushauri kitu pale fikra zako zinapokutana na vikwazo. Siku hazifanani, leo waweza kuwa vizuri lakini kuna siku unaweza kuwa na mawazo, hapo ndipo anapopaswa kutumia nafasi yake kama mke kukurudisha katika hali ya kawaida.
Marafiki zangu, tukubaliane tu kwamba mkeo ndiye mtu pekee ambaye unatumia muda mwingi zaidi kuwa naye karibu. Utakuwa kazini ambako mnashirikiana na wafanyakazi wenzako kwa saa kadhaa  lakini utarudi nyumbani ambako utatumia muda mwingi zaidi kuwa na mwenzako.
Hivyo basi asipokuwa mtu sahihi kwako ni dhahiri kwamba atakuangusha. Lazima uwe na mke ambaye anawaza maendeleo awe anajua anapaswa kufanya nini pindi tatizo linapotokea, asijekuwa mtu wa kulikimbia tatizo.
Awe mvumilivu katika kipindi ambacho uchumi utayumba ndani ya nyumba. Ajue kwamba wewe ndiye mumewe katika hali yoyote. Asije akawa mwepesi kukusaliti kwa sababu tu ameona mpo katika kipindi kibaya kiuchumi.
Badala ya kukusaliti au kukukimbia, anapaswa kufikiri zaidi juu ya mbinu mbalimbali za kujinasua katika tatizo linalowakabili. Badala ya kukaa kusubiri kuletewa kila kitu basi pengine na yeye aweze kubuni miradi midogomidogo ambayo inaweza kupunguza makali ya ugumu wa maisha.
Elimu hii si ya wanaume pekee, wanawake nao wanapaswa kuitumia ili kuweza kujua sifa za mwanaume ambaye anafaa kuwa mumewe. Usikurupuke kuolewa na mtu ambaye huna imani naye au kwa kigezo kwamba pengine ana uwezo wa kifedha.
Lazima ujue ni mtu ambaye anaweza kustahimili shida na raha. Atakuwa bega kwa bega pale wewe utakapohitaji msaada wake? Vinginevyo usikubali, mpe muda wa kutosha kumjua tabia yake. Kama kuna kitu unaona hakipo sawa na kinaweza kurekebishika basi jaribu kumshauri na ukiona hawezi basi ni vyema ukaachana naye usije kujuta baadaye.
Kila mmoja wenu anapaswa kuoa au kuolewa na mtu ambaye anakidhi na hali ya aina yoyote. Ndoa si lelemama, haina majaribio, mkikubaliana basi hakuna kugeuka nyuma!
+

ISHU SI KUOA, ILA UNAMUOA NANI KWA VIGEZO GANI?-1

Na Michael Shuma,Upupu:
VITABU mbalimbali vya dini vinatufundisha umuhimu wa ndoa. Najua wengi tutakuwa tunafahamu juu ya huu mstari ambao upo kwenye Biblia; “Naye mwanamke atamuacha baba na mama yake, ataambatana na mumewe na kuwa mwili mmoja.”
Marafiki zangu, mstari huo una maana kubwa sana. Ndoa ina mapana yake katika maisha ya mwanadamu. Ndoa si kufuliana nguo wala si kufanya tendo la ndoa peke yake. Ndoa inahusisha vitu vingi ambavyo wanandoa inabidi washirikiane.
Ili ndoa idumu, wanandoa lazima wawe wanaendana kwa kila jambo. Waelewane, wavumiliane, wawe na upendo wa dhati na siyo wa kuigiza.Marafiki zangu, kwenye dunia hii iliyojawa na changamoto nyingi, wanandoa wanapaswa kufarijiana, kutiana moyo ili kuweza kuvuka vizingiti na mitihani mbalimbali ya maisha.
Ndoa ni ya watu wawili. Si kitu cha kufuata mkumbo, eti kisa fulani kaoa basi na wewe uoe. Ukioa kwa kufuata fasheni, itakula kwako kama wasemavyo vijana wa kisasa.
Mke ambaye utaishi naye ndani kwa kipindi chote cha maisha yenu lazima awe na sifa za kuwa mke. Ajue kwamba ndoa ina shida na raha, anapoona utamu wake atambue pia kuna uchungu wake, kuna siku shida inaweza kutokea.
Ajue namna ya kukabiliana nayo, hawezi kulikimbia tatizo wakati tayari ameshaingia ndoani.
Wanaume wengi sana wanakosea sana kwenye eneo hili, asilimia kubwa huwa wanaendeshwa na matamanio ya mwili. Anamtamani mwanamke mzuri basi akili yake inaamini kwamba anafaa kuwa mke.
Anasahau kabisa kwamba kuna kitu kinaitwa tabia. Hajiulizi mara mbilimbili kwamba mtarajiwa wake ana tabia njema? Hana muda wa kumtazama mtarajiwa wake kama anaweza kuwa mvumilivu.
Hawazi kabisa kwamba kuna kipindi cha maradhi, anasahau kwamba kuna wakati uchumi unaweza kuyumba ndani ya nyumba, atavumilia?Ili kujua vizuri tabia ya mwenzako lazima utenge muda mzuri wa kumchunguza umpendaye kabla ya kufanya maamuzi. Usikurupuke maana maamuzi ya dakika tano yanaweza kukugharimu maisha yako yote.
Tumia muda mwingi wa kushirikiana na mwenzako ili uweze kumsoma tabia zake. Tabia ya mtu ni kama ngozi, kuibadili ni ngumu sana. Mtu hawezi kuficha tabia yake hata iweje, atadanganya miezi miwili lakini wa tatu atajisahau, utagundua tu.
Utakapoigundua tabia yake ina mapungufu, usikurupuke kumuacha. Muelekeze, mpe muda wa kubadilika na kama ni mtu wa kubadilika, anaweza kubadilika. Ukiona habadiliki katika kipindi fulani basi ni bora ukaachana naye mapema kabla hamjafika mbali ili kuepuka maumivu mazito baadaye.
+

KUNA UBAYA GANI KUFUATILIA NYENDO ZA MPENZI WAKO?


Michael Shuma,Upupu:
Ni wiki nyingine tulivu kabisa tunakutana kupitia safu hii nikiamini umzima na unaendelea nyema na maandalizi ya sikukuu za Christmas na Mwaka Mpya.Mimi namshukuru Mungu kwa kila jambo ambalo amekuwa akinitendea katika kila siku ya maisha yangu na nimuombe tu anijaalie niwe miongoni mwa wale watakaouona mwaka 2015 wakiwa wazima.
Mpenzi msomaji wangu, kilio cha wengi walio kwenye uhusiano ni kusalitiwa na wapenzi wao waliotokea kuwaamini sana. Wapo ambao si tu kwamba wanahisi bali wanawafumania kila kukicha waume/wake zao licha ya imani waliyokuwa nayo kuwa hawawezi kusalitiwa.
Imefika wakati baadhi yetu hatutaki hata kufuatilia nyendo za wenza wetu tukijua kwamba kufanya hivyo ni kujitafutia presha za bure. Labda mimi naweza kuwa na uelewa tofauti katika hili la kufuatilia nyendo za wapenzi wetu. Ninachojua mimi ni kwamba, ili uwe na amani moyoni mwako juu ya mwenza wako lazima uthibitishe kama kweli anakupenda na ametulia.
Utafanya hivyo kwa kufuatilia nyendo zake bila yeye kujua na katika kufuatilia kwako ndipo utajua kama kweli umempata mwenza sahihi ama laa. Wapo ambao husimamia kwenye ule msemo kwamba, ukimchunguza sana bata humli! Jamani ule ni msemo tu, tunajua kila mmoja ana mapungufu yake ila ni vyema ukayajua ya wako ili ujue namna sahihi ya kuishi naye.
Nalazimika kusema haya kwa kuwa, kasi ya wapenzi kusalitiana imekuwa ikishika kasi kila siku kiasi cha baadhi kuhisi bila kusaliti hawasikii raha. Yaani wanapatilizwa kila kitu na wenza wao lakini bado wanatoka nje.
Unakuta mwanaume ana mke mzuri anayejua mapenzi na kila kitu lakini bado mwanaume huyo haridhiki. Pia wapo wanawake ambao wamebahatika kuwapata wanaume ‘handsome’, wanaojua mapenzi na kujali pia lakini bado tamaa za usaliti wanakuwa nazo. Ukiuliza kipi kigeni wanachofuata huko nje, jibu hakuna.
Watu wa sampuli hii ni vyema kuwabaini kuliko kubaki na ile imani kwamba, anakupenda na hawezi kukusaliti. Una ushahidi gani kama kweli anakupenda na hakusaliti huko anakopita?
Hivi leo ukiambiwa utaje sababu inayokufanya uamini kuwa mwenza wako hachepuki utatoa sababu gani? Hakika huwezi kuwa nayo, sanasana utaishia kusema unamuamini kwa kuwa hujawahi kumfumania wala kuona dalili za kuzungukwa.
Kizuri ni kwamba, ukifuatilia sana utagundua wengi wetu hutuna imani ya asilimia 100 ya kutosalitiwa. Wengi wetu licha ya wenza wetu kuonyesha wametulia, bado hatuwaamini kupitiliza. Hii yote ni kwa sababu akiamua kukusaliti anaweza kufanya hivyo na wewe usijue lolote.
Nilishawahi kufanya uchunguzi huko nyuma kwa kuzungumza na baadhi ya watu kuhusu hili suala la kusalitiwa. Wengi walikiri kujua kwamba wanasalitiwa lakini wenyewe wanadai ni mambo ambayo wakiyafuatilia hawawezi kudumu kwenye ndoa zao.
Ni kweli niliobahatika kuongea nao kwenye hili ni wachache sana lakini maelezo yao yamenifanya niwe na uhakika wa hiki ninachokiandika leo.
Kipi kifanyike?
Kutokana na maelezo yangu hapo juu utakubaliana na mimi kwamba hakuna anayeweza kusimama mbele za watu na kuthibitisha kuwa hasalitiwi. Kikubwa ni wewe na mimi kuwaamini wapenzi wetu.
 Lakini pia hakuna ubaya kama utafuatilia na kujua kama kweli uliye naye ametulia na hachepuki. Usibaki kuamini kibubusa kwamba husalitiwi, wakati mwingine fuatilia nyendo zake bila yeye kujua.
Najua kweli ukifanya hivyo unaweza kugundua madudu mengi kwa huyo uliyenaye na ukajikuta unachanganyikiwa lakini ni bora utakuwa umejua yaliyojificha ili uchague mwenyewe kusuka au kunyoa.
Heri ujue kisha kama huwezi kumuacha, uzungumze naye, abadilike kuliko umuache aendelee kufanya ufuska wake gizani kisha wewe ubaki na imani kwamba ametulia na hawezi kukusaliti.
Lakini kama moyo wako unagoma kumfuatilia mpenzi wako na moyo wenyewe unakuhakikishia kwamba mwenza wako katulia, basi baki na imani yako hiyo.Lakini kwa ulimwengu wa sasa kama utakuwa umejihakikishia kwa asilimia 100 kwamba una mpenzi ambaye hajawahi kukusaliti na wala hafikirii, jiweke kwenye kundi la watu waliobahatika na Mungu awabariki sana.
+

SHITUKA WEWE! UTAISHI KWENYE NYUMBA YA KUPANGA MPAKA LINI?

Maisha siku zote ni kuwa na malengo, namaanisha malengo ya muda mfupi na yale ya muda mrefu. Kwamba unaishi huku ukijua mwaka huu utafanya jambo flani na mwaka kesho utafanya jambo flani.
Cha ajabu sasa wapo watu ambao hawana malengo yoyote, wanaishi ili mradi siku zinakwenda.
Hili ni tatizo na ukijaribu kufuatilia utagundua wote wanaoishi bila malengo wana maisha magumu na wameridhika nayo. Yaani hawajui kesho yao itakuwaje na wala hawataki kujishughulisha kujua.
Ilimradi leo Mungu kawajaalia wamekula, wanaona hawana sababu ya kufikiria kesho watakula nini. Hii ni shida!
Katika hilo leo nataka kuwazungumzia wale wenzangu na mimi ambao tunaishi kwenye nyumba za kupanga. Ukifuatilia sana utagundua ni wachache sana ambao hawakuwahi kuishi kwenye nyumba za kupanga, hasa maeneo ya mjini.
Naweza kusema hiyo ni hatua ya tulio wengi katika kuelekea kwenye kumiliki nyumba zetu. Hapa namaanisha kwamba, wengi wetu tumeanza maisha tukiwa tumepanga chumba kimoja, baadaye tukachukua chumba na sebule na hatimaye tukapanga nyumba nzima kadiri vipato vyetu vilivyokuwa vinaongezeka na familia kuwa kubwa.
Lakini katika maisha ya sasa utakuwa ni mtu wa ajabu kama utakuwa unawaza kupanga tu na wala hufikirii siku moja kuwa na nyumba yako na ikiwezekana uwapangishie wengine.  Nasema haya nikimaanisha kwamba, wapo watu huko mtaani ambao wao wamechukulia maisha ya kupanga kama sehemu ya maisha yao. Yaani hawawazi kumiliki nyumba, walipokuwa mabachela, walipanga, walipooa bado waliendelea kupanga na huenda sasa wana familia lakini bado wanapanga na hawana mikakati ya kuwa na ‘mijengo’ yao.
Walio katika mazingira hayo wajue wanajiandaa kuzeeka wakiwa kwenye nyumba za kupanga, jambo ambalo ni baya sana. Ifike wakati ukae na kujiuliza kwamba, wale ambao walianza kwenye nyumba za kupanga lakini sasa wanaishi kwenye nyumba zao huku nao wakiwa na wapangaji wao wana kipato gani kikubwa kukushinda wewe?
Marafiki na wafanyakazi wenzako ambao huenda mnapokea mshahara sawa wamejenga, wewe pesa zako zinaishia wapi? Au unaona kujenga siyo ishu? Kwamba hata usipojenga ilimradi una sehemu ya kuishi na mambo yanakwenda sawa, basi poa?
Mimi nadhani unakosea, kumbuka ipo siku utakuwa huna pesa ya kupanga, nguvu zimeisha na una familia ambayo inahitaji uihifadhi. Kama utakuwa hujajijengea kakibanda kako katika wakati huu ambao una kazi na Mungu anakujaalia unapata vijisenti, huoni ipo siku utajuta?
Mimi nakushauri kwamba, kama unafanya kazi au una vipato vingine na hujajenga, wala huna malengo hayo, ni vyema ukaanza sasa. Weka mikakati ya kuhakikisha unakuwa na nyumba yako. Jinyime kama wanavyofanya wenzako. Kumbuka ni wachache sana ambao walijenga baada ya kupata pesa nyingi, wengi walidhamiria siku moja kuachana na mambo ya kupanga, wakawekeza kidogokidogo, mara wakanunua viwanja, wakaanza msingi na hatimaye kusimamisha nyumba. Sasa wanaishi kwao na wengine ni baba wenye nyumba/mama wenye nyumba, kinachokushinda wewe ni kipi?
Tena mbaya zaidi baadhi ya waliojenga nyumba zao unaweza kukuta wanapata pesa ndogo kuliko hizo unazopata wewe, huoni umefika wakati wa wewe kufikiria kuwa na nyumba yako? Tafakari kisha ni vyema ukachukua hatua.
+

Saturday 6 December 2014

RAHA YA MAFANIKIO YAKO USAIDIE NA WENGINE WAFANIKIWE!

Mpenzi msomaji wangu, unapojaaliwa kuwa na mafanikio jambo la kwanza unatakiwa kumshukuru sana Mungu pamoja na wale ambao kwa namna moja ama nyingine wamekufanya ufike hapo ulipo.Huwezi kufanikiwa kwa ujanja wako, mafanikio yako yote nyuma yake kuna mkono wa Mungu. Yeye ndiye anayeweza kuziona jitihada ulizonazo na akaona akutimizie ndoto zako. Ukiacha yeye, wapo watu mmojammoja au kwa vikundi na taasisi ambao wamechangia wewe kuwa na mafanikio uliyo nayo. Hawa ni watu wa kuwaheshimu sana. Kamwe usiwasahau, endelea kuwa nao karibu kwani umuhimu wao kwako ni mkubwa sana.
Aidha, unapofanikiwa na wewe unatakiwa kuwa chachu ya mafanikio kwa wengine. Unatakiwa kuwashika mkono ndugu, marafiki na watu wengine wanaokuzunguka ili watoke kwenye hali duni walizonazo. Ukifanya hivyo utazidi kupaa kimafanikio na hata siku moja huwezi kuporomoka.
Ipo mifano mengi ya watu ambao wamefanikiwa lakini wanakosa furaha kuwaona watu wanaowazunguka bado wanaogelea kwenye dimbwi la umasikini.Hawa utawaona wakiwa mstari wa mbele kuwasaidia wengine kimawazo na hata kifedha ili nao wainuke na waweze kutimza ndoto zao.
Iko wazi kwamba bosi wangu, Eric Shigongo ni miongoni mwa watu wenye mafanikio makubwa. Kama uliwahi kusoma popote kuhusu historia ya maisha yake, utaona ni jinsi gani amepambana kufika hapo alipo.
Kinachotia moyo zaidi ni kwamba, licha ya mafanikio aliyonayo, hajaridhika, bado anaendelea kupambana na kuzidi kujiwekea malengo makubwa zaidi.
Lakini licha ya mafanikio yake, bosi wangu huyu ambaye pia ni mwalimu wa ujasirimali amekuwa akitumia muda wake mwingi kutoa elimu kwa watu mbalimbali juu ya namna wanavyoweza kutoka kwenye umaskini na kuingia kwenye utajiri.
Amekuwa akifanya hivyo kupitia vitabu vyake, kwenye makongamano na semina mbalimbali akieleza njia ambazo yeye amepita mpaka akafikia hapo alipo sasa. Ukiacha elimu anayotoa, pia amekuwa akiwasaidia wengi kifedha ili waweze kutimiza ndoto zao. Hiki ndicho ambacho watu waliofanikiwa wanatakiwa kukifanya.
Huwezi kuendelea kuwa kwenye mafanikio kama utakuwa mchoyo wa kuwafanya na wengine wafanikiwe. Utakuwa ni mtu wa ajabu kama utakuwa unataka ufanikiwe wewe tu na wengine waendelee kuwa mafukara.
Hivi utakuwa ni mtu wa aina gani kama una pesa nyingi lakini umekuwa mgumu kuwasaidia wale ambao wanahitaji msaada kutoka kwako? Faida ya wewe kufanikiwa ni ipi sasa kwa jamii yako?Mimi nadhani kuna kila sababu ya wale ambao wamefanikiwa kuona wana jukumu la kuwasaidia na wengine kufanikiwa.
Kama si kwa kuwapa mitaji basi hata kwa kuwapa mawazo ambayo yanaweza kubadili fikira zao.
 Usijenge mazingira ya kwamba wewe tu ndiye unayestahili kuishi vizuri, wasaidie na wengine waishi maisha ya furaha. Kumbuka faida ya kufanya hivyo ni kubwa sana.
Kwanza Mungu atakuongezea mafanikio yako na utashangaa kila unalolipanga linatimia. Pia, jamii inayokuzunguka itakupenda na itakuona ni mtu unayejali wengine.
Kwa maana hiyo unapofanikiwa usijitenge na jamii inayokuzunguka. Saidia pale inapopidi, washike mkono wengine waweze kusimama. Kumbuka siku wakiwa wamefanikiwa, ile tu kusema ‘flani kanisaidia mimi kufika hapa’, Mungu anakuzidishia baraka na unashangaa mambo yanazidi kukunyookea.
+

Friday 5 December 2014

Texting Really Hurts Your Spine!

We’ve heard about the dangers of texting for years now. At first, some people complained about text messages, saying that they were a cheap replacement for phone calls and were highly unprofessional and impersonal. There were those who didn’t believe texting would ever really catch on. I needn’t have to argue that texting is incredibly popular now, and that it’s probably more popular than ever; as such, health experts are warning us of another potential problem of constant texting – spinal issues. That’s correct – a back surgeon from New York has done all kinds of research on the subject, and he’s convinced that the way we normally text, by looking down at our phones, exerts around 60 pounds of additional force on our heads. Given the fact that many Americans spend somewhere in the ballpark of an hour a day texting anyone and everyone, over time, that pattern can really have a damaging impact on the spine. If left unchecked, it can ultimately lead to back surgeries, etc. Texting Really Hurts Your Spine!
I realized people texted a lot, but I must admit I never thought it could lead to spinal problems. And then, I stumbled across a special on the subject while watching the news the other day. It appears the only way one can “safely” text is by holding the phone directly across from your face, without angling your head whatsoever.
How long do you spend texting each day? Have you suffered any spinal problems directly related to texting? If so, please tell us about them in the comments section below. It will be interesting to see how common this problem really is!
+