Showing posts with label afya. Show all posts
Showing posts with label afya. Show all posts

Wednesday 17 December 2014

JINSI YA KUONDOA MADOA YA CHUNUSI

JUISI YA LIMAO NA MAJI YA ROSE
Chukua maji ya rose kiasi kama ni kijiko kimoja na maji ya limao nayo yawe kijiko kimoja paka eneo liloathiriwa na madoa, kaa kwa muda wa nusu saa mpaka saa moja kisha osha uso wako, fanya hivyo kwa muda wa wiki tatu utapona madoa doa yote usoni.
Juisi ya limao na liwa
Chukua juisi ya limao kiasi changanya na liwa kisha paka eneo lililoathirika, kaa kwa muda wa dakika tano utaona matokeo.
Juisi ya limao na unga wa mdalasini pia ni tiba nzuri ya kusafisha uso kuondokana na madoa yote.
Asali na mdalasini
Chukua vijiko vitatu vya asali na kimoja cha mdalasini changanya kisha paka usoni pia ni tiba nzuri inasaidia kwa kiasi kikubwa.
Apple na asali
Chukua apple liponde changanya na asali kiasi, kisha paka usoni mbali na kutibu madoa pia inatibu chunusi.
Maji ya kitunguu swaumu
chukua maji ya kitunguu swaumu paka kwenye madoa yote utaona matokeo.
Nyanya
chukua kipande cha nyanya paka usoni kisha kaa kwa muda wa saa moja nayo ni tiba nzuri.

Tango
Tango pia ni tiba, chukua kipande sugua uso wako kila siku asubuhi utaona matokeo.
Papai
Chukua papai liponde kisha paka usoni litakusaidia kuondoa tatizo la madoa yote usoni.
+

VIJUE VYAKULA BORA NA FAIDA ZAKE MWILINI


TUNAAMBIWA kuwa kuishi vizuri ni pamoja na kula chakula bora na sahihi. Pia, mtu anayeishi vizuri ni yule ambaye hasumbuliwi na maradhi hatari na njia pekee ya kuulinda mwili dhidi ya maradhi hatari ni kujua ipasavyo na kuvitumia vyakula bora pamoja na kufanya mazoezi.
Katika makala yafuatayo, nitakuorodhoshea baadhi ya vyakula vinavyotajwa kuwa bora (super foods) ambavyo faida zake mwilini vimeanishwa. Kwa mlaji, linakuwa jambo la busara kujua faida ya kila chakula unachoingiza tumboni. Kwa mujibu wa mwandishi wa makala kuhusu vyakula hivi bora, Bw.Hakeem Rahman, hivi ni vyakula vinavyowafanya “wenye afya nzuri kuendelea kuwa na afya nzuri zaidi na wenye afya mbovu, kuwa na afya nzuri.”
SAMAKI
Wana virutubisho aina ya Omega 3 ambavyo huulinda moyo dhidi ya maradhi. Samaki pia wana virutubisho vinavyomuongezea mlaji uwezo wa kukumbuka (memory), kuna virutubisho vyenye uwezo wa kupambana na kansa mwilini, kuongeza kinga mwilini na kuondoa mafuta mabaya mwilini (Bad cholesterol). (unashauriwa kula samaki kwa wingi kadiri uwezavyo).
Baadhi ya virutubisho muhimu vinavyopatikana kwenye samaki ni pamoja na vitamini D, vitamin 12, vitamini B3, vitamini B6,  Omega 3 Fatty acids, protini na madini mengine mengi.
KARANGA
Unaweza ukazidharau karanga, lakini zina faida kubwa mwilini. Miongoni mwa faida zake ni pamoja na kuimarisha afya ya moyo, hupunguza kolestro mbaya mwilini na kuongeza kolestro nzuri. Mafuta mazuri yaliyomo kwenye karanga hupunguza shinikizo la juu la damu na huponya magonjwa ya moyo na hupunguza uzito. Faida zote hizi unaweza kuzipata kutoka kwenye karanga au siagi iliyotengenezwa kutokana na karanga (peanut butter). (unashauriwa kula kiasi kadhaa kila siku, hasa za kuchemsha ndiyo nzuri).
KAROTI
Miongoni mwa faida nyingi za karoti ni pamoja na kushusha kolestro mbaya mwilini, kupunguza unene, kuimarisha nuru ya macho, kuimarisha shinikizo la damu, inatoa kinga kwenye figo na inaimarisha sukari mwilini. (kula kadiri unavyoweza, mbichi au zilizochemshwa).
MAHARAGE YA SOYA
Haya ni maharage bora kabisa ambayo yana faida nyingi mwilini, ikiwemo kushusha shinikizo la damu, kuimarisha sukari mwilini, kupambana na ugonjwa wa kisukari, figo, moyo, kutoa kinga dhidi ya ugonjwa wa kansa ya kibofu na magonjwa mengine ya wanawake.
PAPAI, TIKITI MAJI
Miongoni mwa matunda muhimu mwilini ambayo hata mgonjwa wa kisukari anashauriwa kuyala ni pamoja na papai na tikitimaji ambayo yanaelezwa kuwa na kiwango kikubwa cha ufumwele (fibre) na hivyo kutoa mchango mkubwa sana katika kuimarisha kiwango cha sukari mwilini. (kula kiasi cha moja katika ya matunda hayo mawili, kila siku).
KITUNGUU SAUMU
Hiki ni kiungo cha mboga, licha ya kuonekana kama ni kiungo cha kuongezea ladha tu ya chakula, lakini ni miongoni mwa vyakula vyenye faida kubwa katika afya zetu. Kitunguu saumu husaidia kuyeyusha damu mwilini hivyo kumuepusha mlaji kushikwa na ugonjwa wa moyo pamoja na presha. Kitunguu hicho pia hutoa kinga kwenye ini na huondoa maumivu ya viungo. Kula angalau kitunguu kimoja mara moja kwa wiki.
+

IJUE TIBA YA UKOSEFU WA CHOO



UKOSEFU wa choo kwa muda mrefu ni tatizo linalowakabili watu wengi, lakini kwa bahati mbaya sana miongoni mwa watu wenye tatizo hili hawajui kama lina madhara makubwa na huweza kuwa chanzo cha ugonjwa mkubwa baadaye unaoweza kusababisha hata kifo.
Kwa kawaida, binadamu anatakiwa kwenda haja kubwa kila siku, angalau mara moja kama siyo zaidi ya mara moja, kulingana na aina ya chakula na kazi anazozifanya kwa siku. Anapopitisha siku moja bila kwenda haja kubwa, ili hali amekula kama kawaida, aelewe kwamba kuna dosari tumboni.
Madhara ya ukosefu wa choo kwa muda mrefu ni pamoja na kupatwa na maumivu makali ya tumbo, magonjwa ya moyo, kupatwa na kiharusi na kujikunja kwa utumbo ambako huweza kusababisha kifo kama hali hiyo haitaweza kushughulikiwa mapema na kwa usahihi.
Kujiepusha na madhra yatokanayo na ukosefu wa choo wa muda mrefu ni rahisi sana. Ili kujiepusha na tatizo hilo, unatakiwa kuzingatia kanuni ya kwanza ya KUNYWA MAJI kwa wingi kila siku. Hakikisha kwa siku unakunywa maji ya kutosha, kiasi cha lita moja hadi lita tatu au zaidi, kutegemeana na kazi unazozifanya.
Aidha, kanuni ya pili, ambayo nayo ni rahisi ukilinganisha na madhara utakayoweza kuyapata kwakuacha kuifuata, ni ulaji wa vyakula vyeye kamba lishe ya kutosha (fibre). Utapata kamba lishe ya kutosha kwa kula matunda na mboga za majani kwa wingi. Matunda kama parachichi, machungwa, embe, papai, nafaka zisizokobolewa ni miongoni mwa matunda na vyakula vyenye ‘fibre’ za kutosha.
Usidhani ulaji wa matunda na mboga za majani ni anasa, bali ni jambo la lazima kwa sababu ni uhai wako. Kwa kunywa maji mengi, kutarahisisha usagaji wa chakula tumboni na kufanya upitaji wa sumu na uchafu mwingine kwenye utumbo wakati wa kutoka kama haja kubwa kuwa rahisi na laini.
Kwa muhtasari unaweza kusema chanzo kikubwa cha ukosefu wa choo ni tabia ya kutokupenda kunywa maji mengi na kutokula matunda, mboga za majani pamoja na nafaka zisizo kobolewa mara kwa mara, kama siyo kila siku. Kwa upande mwingine, adui mkuwa wa ukosefu wa choo, ni maji na lishe ya matunda na mboga za majani pamoja na nafaka zisizokobolewa.
Hivyo, utendee haki mwili wako nao ukutendee haki kwa kukulinda dhidi ya maradhi hatari kwa kupenda kunywa maji ya kutosha kila siku, bila kujali kama unasikia kiu ama la, kwani maji ni uhai na ni tiba bora kuliko zote.
+

VYAKULA HATARI VYA KUOGOPA


Kila siku tupo katika kujifunza. Hakuna mwanadamu yeyote aliyezaliwa akiwa anajua kila kitu. Kujifunza ni wajibu wa kila binadamu na hasa kujifunza mambo muhimu yanayohusu maisha yetu ya kila siku.

Katika kujifunza masuala ya vyakula bora na visivyo bora, katika makala yetu ya leo tunajifunza baadhi ya vyakula ambavyo si salama kwa afya zetu, hata kama tumekuwa tukidhani hivyo kwa miaka yote iliyopita.

Baadhi ya vyakula vifuatavyo, vimethibitika kuwa na madhara katika afya ya binadamu na tumeshauriwa kuviepuka. Ingawa ni vyakula tunavyovitumia kila siku, lakini inatupasa sasa kukubali tulikuwa hatujui na sasa tumejua, hivyo tuviepuke:

NYANYA YA KOPO (Canned Tomatoes)
Kwa mujibu wa mtaalamu Fredrick vom Saal (PhD) wa Chuo Kikuu cha Missouri nchini Marekani, utengenezaji wa kopo la kuhifadhia nyanya kwa ndani, hutumia kemikali aina ya ‘bisphenol-A’ ambayo inaaminika kuwa chanzo cha matatizo ya uzazi, magonjwa ya moyo, kisukari na unene pamoja na gesi tumboni (acidity).

Mbali na kopo lenyewe kutokuwa salama, ili kuihifadhi nyanya isiharibike haraka, lazima iongozewe vitu (additives) na kuwekewa kemikali za kuhifadhia chakula (preservatives) ambavyo navyo kwa ujumla wake siyo salama kiafya. Kwa msingi huo, huna sababu ya kutumia nyanya za kopo wakati nyanya halisi zipo tele sokoni.
NYAMA YA NG’OMBE WANAOLISHWA MAHINDI (Corn- Fed Beef).

Kwa mujibu wa mtaalamu Joel Salatin kutoka Kampuni ya Polyface Farms na mwandishi mashuhuri wa vitabu kuhusu kilimo bora chini Marekani, ng’ombe kwa kawaida ameumbwa kuishi kwa kula majani, siyo nafaka.

Lakini sasa wafugaji huilisha mifugo yao nafaka, ikiwemo soya na kufanya mifugo kunenepeana kuliko kawaida, kwa lengo la kuchinja ng’ombe walionona ili kujipatia faida zaidi. Nyama itokanayo na mfugo wa aina hiyo inakosa uhalisia wake na hivyo kuwa na madhara kwa mlaji.

Katika utafiti mmoja uliofanywa hivi karibuni, imebainika kuwa ukilinganisha na ng’ombe wanaolishwa nafaka, wale wanaolishwa majani, nyama zao zina kiwango kingi cha virutubisho kama vile Carotene, Vitamin E, Omega 3, Calcium, Magnesium na Potassium.

VIAZI VYA KUOTESHWA KWA MBOLEA (Non Organic Potatoes)
Kwa mujibu wa mtaalamu Jeffrey Moyer, Mwenyekiti wa Bodi ya masuala ya vyakula asilia, vyakula vyote vitokanavyo na mizizi (viazi, mihogo, n.k) havitakiwi kuoteshwa kwa mbolea wala kumwagiliwa dawa za kuulia wadudu (pesticides), kwa sababu vina kawaida ya kunyoya ardhini kemekali hizo.

Ulimaji wa kisasa kwa baadhi ya wakulima, hasa katika nchi zilizoendelea, viazi huoteshwa kwa kutumia mbolea, humwagiliwa dawa za kuulia wadudu na hata wakati wa kuchimba na kuvuna, bado viazi hivyo huwekewa tena dawa za kuzuia visiote au kuharibika. Ulimaji huu hukifanya kiazi au muhogo kuwa sumu.

Hivyo basi, inashauriwa tulime viazi na mihogo kwenye udongo wenye rutuba ya asili au kwa kutumia mbolea asilia, kama vile majani au kinyesi cha ng’ombe na tuepuke kutumia mbolea nyingine zenye kemikali au sumu. Kwa kufanya hivyo tutakula viazi na mihogo na kupata faida ya vyakula hivyo asilia.

MAZIWA YA NG’OMBE WALIOLISHWA DAWA (Milk Produced with artificial hormones)
 Mtaalamu Rick North anayejishughulisha na masuala ya vyakula salama anasema kuwa baadhi ya wafugaji wa ng’ombe wa maziwa huwalisha ng’ombe wao vichocheo bandia vya mwili (artificial hormones) vya kuzalisha maziwa (rBGH or rBST) ili kuifanya mifugo yao izalishe maziwa mengi.

Kitendo hicho, hufanya maziwa yatokanayo na ng’ombe aliyelishwa vichecheo hivyo kutokuwa salama na inaelezwa kuwa maziwa ya aina hiyo pia yameonekana kusababisha saratani za matiti, kibofu cha mkojo na tumbo kwa mnywaji.

Hivyo chonde chonde wafugaji wa mijini, walisheni ng’ombe wenu wa maziwa vyakula vya asili walivyoumbiwa na Mungu, ambavyo ni majani na siyo madawa kwa sababu ni hatari kwa afya ya mlaji.
+

JINSI YA KUGUNDUA MAAMBUKIZI KWENYE UZAZI (DIAGNOSIS OF PID)

Baadhi ya wagonjwa watahitajika kulazwa hospitali ambapo watapewa dawa za saa na kuwa chini ya uangalizi wa haraka wa manesi na madaktari.Wagonjwa wanaohitaji kulazwa ni kama wale wanaodhaniwa kuwa wana uvimbe au jipu kwenye mfuko wa mayai yaani tube ovarian abscess au wale wenye kutapika sana na wenye homa kali pia wenye maumivu makali ya tumbo yanayofanana na kidole tumbo. Wagonjwa ambao hawakupata nafuu baada ya matumizi ya dawa ya awali baada ya saa 48 ya kumaliza dawa na wale walioshindwa kumeza dawa pia wagonjwa wenye rirusi vya ukimwi watahitajika kulazwa.
Dawa zinazotumika kwa wale waliolazwa ni kama vile cefoxitin na clindamycine ikichanganywa na gentamycine.Nafuu ya mgonjwa itajulikana baada ya mgonjwa kujisikia vizuri na homa itashuka,  pia maumivu ya tumbo yatapoa na vipimo vya maabara vitaonyesha kuwa vijidudu vimeisha.
Baadhi ya wagonjwa watahitaji upasuaji kama kutakuwa na madhara makubwa (complications) kama vile vijidudu kuingia kwenye utumbo, jipu kwenye viungo vya uzazi (pelvic abscess) usaha kwenye mfuko wa mayai (turbo ovarian abscess).
JINSI YA KUJIKINGA (PREVENTION)
Kwanza, matabibu wana wajibu wa kuelimisha jamii juu ya maambukizi yanavyotokea na kujiepusha nayo.
Pili, jamii iepushwe mwanamke kuwa na uhusiano wa kingono na wanaume wengi (multiple sexual partiners) na watu wajue matumizi sahihi ya kondom.
Mwanamke lazima amlete mwenza wake ili aweze kufanyiwa vipimo vya uhakika na akithibitika hana maambukizi ya kisonono basi ataweza kupewa dawa za kuua vijidudu vya clamydia maana ni vigumu kuweza kugundua vijidudu vya clamydia. Mwenza wake yaani atumie dawa kwa muda wa siku saba.
Ufuatiliaji wa mgonjwa kwa kumpima  ufanyike baada ya wiki moja baada ya wote kutibiwa.
Kwa mwanamke apimwe kila anapomaliza hedhi na majibu yaonyeshe kuwa hana ugonjwa, upimaji ufanyike mara tatu mfululizo na majibu yaonyeshe kuwa hana ugonjwa. Mtu yeyote atakayejihisi ana tatizo hili asitumie dawa hizo bila kuonana na daktari ambaye atampima.
+

Friday 5 December 2014

Texting Really Hurts Your Spine!

We’ve heard about the dangers of texting for years now. At first, some people complained about text messages, saying that they were a cheap replacement for phone calls and were highly unprofessional and impersonal. There were those who didn’t believe texting would ever really catch on. I needn’t have to argue that texting is incredibly popular now, and that it’s probably more popular than ever; as such, health experts are warning us of another potential problem of constant texting – spinal issues. That’s correct – a back surgeon from New York has done all kinds of research on the subject, and he’s convinced that the way we normally text, by looking down at our phones, exerts around 60 pounds of additional force on our heads. Given the fact that many Americans spend somewhere in the ballpark of an hour a day texting anyone and everyone, over time, that pattern can really have a damaging impact on the spine. If left unchecked, it can ultimately lead to back surgeries, etc. Texting Really Hurts Your Spine!
I realized people texted a lot, but I must admit I never thought it could lead to spinal problems. And then, I stumbled across a special on the subject while watching the news the other day. It appears the only way one can “safely” text is by holding the phone directly across from your face, without angling your head whatsoever.
How long do you spend texting each day? Have you suffered any spinal problems directly related to texting? If so, please tell us about them in the comments section below. It will be interesting to see how common this problem really is!
+