Showing posts with label udaku. Show all posts
Showing posts with label udaku. Show all posts

Wednesday 4 March 2015

SERENGETI BOY: NIMELIFAIDI PENZI LA WOLPER!


Akizungumza na GlobalTV Online kwenye mahojiano maalum juzikati, dogo huyo alisema kuwa katika maisha yake ya kimapenzi hakuna mwanamke ambaye aliwahi kutoka naye na kujiachia kwa furaha kama ilivyo kwa Wolper.
Fredy Felix kutoka Makomando.
“Kiukweli msichana pekee ambaye nimewahi kuwa naye katika mapenzi na kumpenda kwa dhati ni Wolper pekee.“Mara yangu ya kwanza kukutana naye ilikuwa kama ‘sapraiz’ vile (habari zinasema kwamba walikutana maeneo ya Kinondoni), alipoingia kwangu nashukuru naye alinipenda na kunifanyia kila nilichohitaji.
Staa wa Bongo Movies, Jacqueline Walper Massawe ‘Wolper.
“Nampenda sana Wolper na kila siku nimekuwa nikiahidi kwamba huyo ndiye mwanamke pekee ambaye nitakuja kuishi naye hata kama ni uzeeni maana ninampenda kutoka moyoni.“Sidhani kama moyo wangu utampenda mwanamke mwingine kama nilivyompenda Wolper. Kiukweli niliinjoi sana penzi lake,” alisema Fredy huku akijutia kumwagana naye bila sababu ya msingi.
Alipotafutwa Wolper ili kupata undani wa ishu hiyo simu yake ilipokelewa na aliposomewa mashtaka yake alikaa kimya bila kujibu chochote. Hata hivyo jitihada za kumtafuta zinaendelea.
+

Monday 2 March 2015

LINAH & RECHO WAFANYA MAMBO YA AIBU KWEUPEE

Estelina Sanga ‘Linah’ na shostito wake, Winfrida Josephate ‘Recho’ wakilishana keki kwa mdomo.
Hamnazo? Masistaduu wa Bongo Fleva, Estelina Sanga ‘Linah’ na shostito wake, Winfrida Josephate ‘Recho’, wamefanya mambo ya aibu mbele ya kadamnasi.
Tukio hilo la aibu lililoshuhudiwa na Ijumaa Wikienda, lilijiri hivi karibuni usiku kwenye bwawa la kuogelea (swimming pool) ndani ya Hoteli ya Regency-Mikocheni jijini Dar ambapo kulikuwa na ‘bethidei’ ya Recho.Awali, mastaa hao walianza kwa kulishana keki kwa staili ya njiwa (kwa mdomo), jambo lililoibua minong’ono mahali hapo.
Winfrida Josephate ‘Recho’.
Kama haitoshi, baada ya tukio hilo, wawili hao waliweka mapozi tata wakipiga picha zilizowaonesha nusu utupu huku vinguo walivyovaa vikiacha wazi sehemu kubwa ya maumbile yao nyeti.
“Duh! Hawa watoto sasa ni too much, waone walivyojiachia na vivazi vya aibu, yaani hawatazamiki mara mbili,” alisikika mmoja wa wahudhuriaji wa pati hiyo.Baada ya kunasa tukio hilo, mwana-habari wetu aliwafuata wawili hao kutaka kujua kulikoni kujiachia kihasara-hasara ambapo waliomba waachwe wafanye yao
+

JAMAA AKUTWA AMEKUFA, MAITI YAKE YALIWA NA PAKA!

Mwisho wa enzi! Jamaa mmoja aliyetambuliwa kwa jina moja la Mbulu amekutwa kwenye jumba bovu akiwa amekufa kisha mwili wake kutoa harufu kali huku ukiliwa na paka.
Mwili wa Mbulu ukitolewa ndani ya jumba bovu.
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, maiti ya jamaa huyo iligundulika wikiendi iliyopita katika jumba hilo maeneo ya Mtaa wa Simu B Kata ya Mji Mpya mkoani hapa ambapo wananchi wa maeneo hayo walisikia harufu kali kutoka kwenye jumba hilo, walipoingia ndipo wakakuta mwili wa jamaa huyo huku pua na sehemu za uso zikiwa zimetafunwa na paka.
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, mwenyekiti wa mtaa huo, Maneno Kifea ’Ticha’ alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.Licha ya harufu kali mwanahabari wetu alijitosa na kuingia kwenye jumba hilo ambapo alishuhudia mwili wa jamaa huyo ukiwa umeharibika.
...Mwili ukipakizwa kwenye gari.
Hata hivyo, serikali ya mtaa huo ilitoa taarifa polisi ambao walifika na kuuchukua kisha kwenda kuuhifadhi kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro huku uchunguzi ukiendelea juu ya kifo chake.  
+

KUMBE SHAMSA ALIKUTANA NA MUMEWE KIAJABU



STAA wa filamu Bongo, Shamsa Ford amefungukia uhusiano wake kwa mara ya kwanza na mumewe, Dickson Matoke kwamba walikutana kiajabuajabu na kuwa wapenzi.
Staa wa filamu Bongo, Shamsa Ford
Akizungumza katika mahojiano maalum na Kipindi cha Me and You With Love kilichofanywa na Global TV hivi karibuni, Shamsa alisema kuwa siku ya kwanza hakudhani kama Dick ndiye atakuwa mumewe kwani walikuwa wakikutana katika kumbi za starehe tu.
“Siku ya kwanza tulibadilishana namba na ukawa ndiyo kama mchezo, kila tukitaka kwenda kwenye starehe alikuwa akinipigia simu hadi ikawa mazoea na kujikuta tukiangukia katika penzi,” alisema Shamsa.
Shamsa ameongea mengi kuhusiana na mapenzi na maisha yake kwa ujumla. Mahojiano kamili yatapatikana Alhamisi ya wiki hii kupitia
+

DULLY ANASWA NA TOTOZ KLABU YA USIKU!

Kha! Hata kabla ya siku 40 baada ya kifo cha baba yake, Ebby Sykes aliyefariki wiki mbili zilizopita, legendary wa Bongo Fleva, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ amenaswa klabu ya usiku akiwa na totoz za kumwaga hivyo kuibua minong’ono na mshangao ikidaiwa kwamba ni mapema mno kujirusha.
Legendary wa Bongo Fleva, Abdul Sykes ‘Dully Sykes’ akiwa na totoz.
Staa huyo wa Ngoma ya Togola alinaswa na Ijumaa Wikienda ndani ya Club East 24 iliyopo Mikocheni jijini Dar, wikiendi iliyopita ambapo jamaa alikuwa bize akifanya yake bila kujali mashabiki waliokuwa wakimshangaa wakati B-Band chini ya Banana Zorro ikifanya makamuzi.
Wakati makamuzi ya bendi hiyo yakiwa yamepamba moto, Dully alionekana akikumbatiwa kimahaba na mrembo mmoja baada ya mwingine.
Akijiachia na moja ya totoz hizo.
“Jamani yule si Dully ambaye amefiwa na baba yake juzi tu? Mbona amegandana na yule mrembo kule ukutani? Hebu waangalie wanafanya nini jamani? Duh! Kweli haya ni mambo ya kizungu,” alisikika mdada mmoja aliyeonekana kuwapiga chabo kwenye giza huku akimsisitiza mwenzake naye apige chabo.
Kufuatia tukio hilo, mwanahabari wetu alimfuata Dully kisha akampa pole na kumuuliza kulikoni kujivinjari klabu usiku huo uliokuwa ukielekea mishale ya saa nane na ushee?
Akizungumza na Ijumaa Wikienda, Dully alipokea pole kisha akamwaga utetezi wake:
“Nimetokea kwenye kikao cha kupanga hitima ya marehemu baba, nimeona nipitie hapa kupoza machungu ya msiba na kumsalimia swahiba wangu, Banana Zorro.”
Wadau waliokuwa ukumbini hapo walisema ni kawaida kwa mtu mwenye mawazo kujivinjari sehemu kama hiyo kupunguza mawazo na haina maana kujifungia ndani na kulia.
+

Tuesday 3 February 2015

HIVI NDIVYO MUME ALIVYOMCHINJA MKEWE HOTELINI

HUU ni ukatili namba moja kwa wanandoa duniani! Bado picha haijatoka kichwani kwa wakazi wa Manzese jijini Dar kufuatia kifo cha kuchinjwa cha  Josephine Ndengaleo Mushi kinachodaiwa kufanywa na mume wake wa ndoa, Remy Joseph (35).
Remy Joseph (35) anayetuhumiwa kumuua mke wake, Josephine Ndengaleo Mushi.
Tukio hilo la kutisha kusimuliwa achilia mbali kuona, lilijiri saa 9: 10 alasiri ya Januari 29, mwaka huu ndani ya chumba kimoja kilichopo ghorofa ya pili ya  Hotel Friend’s Corner Ltd iliyopo Manzese Argentina, Dar.
KAMA KAWAIDA YA GAZETI LA UWAZ!
Kama kawaida ya Gazeti la Uwazi, kufuatilia matukio makubwa ya kutisha, kusikitisha na hata kufichua maovu. Baada ya habari za mauji hayo kusambaa kama moto wa kifuu, waandishi wetu walianza kuichimba habari hii kwa kina.
SIKU MOJA KABLA YA TUKIO
Kwa mujibu wa mhudumu mmoja wa hoteli hiyo, Januari 28, mwaka huu, Remy na Josephine walifika kwenye hoteli hiyo na kuchukua chumba. Walionekana wenye amani, kwani hakuna sura iliyoonesha kuna tatizo.
“Walikuwa kama wateja wengine. Tena niliwauliza kama wanatoka mkoa, wakasema ni wakazi wa Dar es Salaam, wao ni mke na mume kwa ndoa, waliamua kulala hapa ili kuimarisha mapenzi yao, si lazima kila siku nyumbani,” alisema mhudumu mmoja.
JANUARI 29, SAA 9 ALASIRI, DAMU ZAONEKANA
Kwa mujibu wa baadhi ya wahudumu wa hoteli hiyo, siku ya pili, muda wa saa tisa alasiri, walishtuka kuona damu nyingi ikitoka ndani ya chumba walichopanga wawili hao.“Tulishtuka sana. Tukajua kuna kitu kikubwa kimewapata. Ilibidi tuwagongee mlango ili tujue kilichowapata lakini mlango haukufunguliwa,” alisema mhudumu mwingine.
Mtuhumiwa Remy Joseph akiwa chini ya ulinzi mkali.
POLISI WAITWA
Kwa vile ukimya ulitawala ndani ya chumba hicho huku damu zikiendelea kutiririka, ilibidi uongozi wa hoteli hiyo yenye sifa ya ulinzi, uwasiliane na Kituo cha Polisi cha Ndugumbi ambacho kipo jirani.
Polisi walifika, wakagonga mlango kwa muda mrefu bila kufunguliwa mpaka baadaye sana ambapo mlango huo ulifunguliwa na mwanaume akiwa ameshika kisu mkono wake wa kuume.
POLISI WATUMIA MBINU YA KIVITA
Ndani ya chumba kulionekana damu zimetapakaa kila sehemu. Polisi walimsihi mwanaume huyo kuangusha kisu chini ili waongee lakini jamaa aligoma.
“Polisi walimwamuru mwanaume atupe kisu chini, akakataa. Sura yake wakati huo ilikosa mwonekano wa ubinadamu. Ndipo askari mmoja alitumia mbinu ya kivita, alimpiga mkono wake wa kulia kwa kumshutikiza kisu kikaangukia mbali, akawekwa chini ya ulinzi. Kumbe kile kisu mbali na kumuua mkewe alikitumia kujaribu kujichinja koo lakini ikashindikana,” alisema mhudumu huyo.
MWILI WA MAREHEMU WAKUTWA UMEPIGISHWA MAGOTI
Mwanaume akiwa chini ya ulinzi na pingu mikononi, polisi waliingia chumbani na kukuta damu kila mahali. Cha kusikitisha zaidi, mwili wa marehemu Josephine ulipigishwa magoti, sehemu ya miguu mpaka magoti ikiwa sakafuni na kifuani kulalia kitanda. Halafu ulifunikwa shuka.“Kwa mbali ungeweza kusema kuna binadamu anasali kwa namna ambavyo marehemu huyo alivyokuwa amepigishwa magoti,” alisema mhudumu huyo.
ALITAKA KUJINYONGA
Katika hali iliyoonesha kuwa, mtuhumiwa baada ya kutenda ukatili huo alitaka kujinyonga, polisi walikuta waya wa umeme wa tivii ukining’inia kwenye pangaboi lakini ukiwa umekatika.
Remy Joseph akichukuliwa na Polisi kuchukuliwa hatua za kisheria.
UCHUNGUZI WA POLISI CHUMBANI
Polisi walifanya uchunguzi chumbani na kugundua kuwa, marehemu Josephine alichinjwa shingoni, akakatwa mbavu mbili, moyo na maini vilikuwa nje ‘vikimwagika’, mwisho alichomwa kisu utosini.
LAINI ZA SIMU ZAKUTWA ZIMEKATWAKATWA
Pia kwenye chumba hicho, polisi walikuta simu mbili, ya marehemu na ya mtuhumiwa zikiwa zimeharibiwa laini kiasi cha kukosa mawasiliano.
UWAZI LAZUNGUMZA NA MTUHUMIWA
Uwazi lilipata bahati ya kuzungumza na mtuhumiwa huyo kabla ya kupelekwa Kituo cha Polisi Magomeni, Dar ambapo alisema Josephine alikuwa mke wake na wameishi kwa muda zaidi ya miaka kumi na kupata watoto wawili. Hata hivyo, hakuongea zaidi ya hapo.
UONGOZI WA HOTELI WATOA NENO
Msimamizi mkuu wa hoteli hiyo aliyejitambulisha kwa jina la Zuberi Hussein alipohojiwa na Uwazi alisema:
“Tuliwapokea hawa watu kama wateja wengine. Walilipa shilingi elfu kumi na tano kwa chumba.  Hatukujua kama haya yangetokea, wahudumu ndiyo walibaini baada ya kuona damu ikitiririka mlangoni.”
MWILI WA MAREHEMU WAPELEKWA MUHIMBILI
Baadaye, polisi waliupakiza mwili wa marehemu kwenye gari kuupeleka Hospitali ya Taifa Muhimbili huku mtuhumiwa akipelekwa Kituo cha Polisi Magomeni jijini Dar pembeni yake akiwa amelala marehemu mkewe.
WANACHOJUA NDUGU WA MAREHEMU
Baada ya hapo, Uwazi lilifunga safari hadi eneo la Studio, Kinondoni, Dar nyumbani kwa David Ndeshao Mushi ambaye ni kaka wa marehemu na ndiko sehemu ulipowekwa msiba.
Baadhi ya ndugu wa marehemu walidai kwamba, Josephine na mumewe mara kwa mara walikuwa na migogoro  ya ndoa.
“Ndoa yao haikutulia, walikuwa wanapatanishwa lakini baada ya muda mfupi wanaanza tena ugomvi. Mumewe alikuwa akimhisi vibaya mke wake. Hata hivyo, Desemba mwaka jana, Josephine alienda kuishi kwa kaka yake kutokana na ugomvi,”alisema mmoja wa wanandugu wa karibu.
Kaka mtu  huyo alipohojiwa alisema: “Marehemu alirudi kwangu lakini tulikuwa hatujaongea naye kuhusu ugomvi wao. Nilisafiri mkoani nikamuacha, niliporudi, Jumatano alienda kazini lakini hakurudi. Tulipopiga simu yake akawa hapatikani. Mumewe naye akawa hapatikani hadi taarifa ilipotufikia kwamba kauawa hotelini.
“Tunatarajia kusafirisha mwili kwenda Moshi, Jumapili (juzi). Mazishi yatakuwa Jumatatu (jana). Marehemu ameacha watoto wawili ambao walikuwa wakiishi Tabata, Dar.”
MTUHUMIWA, MAREHEMU
Inadaiwa kuwa, mtuhumiwa alikuwa mfanyakazi wa Baa ya Break Point iliyopo jijini Dar. Marehemu alikuwa mfanyakazi katika Kampuni ya TAC iliyopo Upanga, Dar.
Mmoja wa marafiki zake wa karibu alisema Jumatano mchana, mumewe alimfuata kazini na wakawa na mazungumzo, alimtaka waondoke lakini marehemu alikataa.Alimbembeleza sana mwishowe wakakubaliana na kuondoka lakini wakashangaa kusikia alimuua hotelini.
+

Saturday 3 January 2015

DIAMOND PLATNUMZ AFUNIKA SIKU YA MWAKA MPYA KIGALI, RWANDA

Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ akiwa amebebwa na wacheza shoo wake siku ya mwaka mpya Kigali, Rwanda.
Diamond Platnumz akifanya yake.
Nyomi ya kufa mtu waliofika siku ya shoo hiyo.
Akifanya yake na wacheza shoo wake.
Mfanyabiashara mrembo na muimbaji wa Uganda, Zarinah Hassan 'Zari'  au 'The Boss Lady' mpenzi mpya wa Diamond Platnumz akiwa katika pozi.
Muonekano wa siku ya shoo hiyo.
Diamond Platnumz (katikati) akifanya yake akiwa na Yamoto Bendi.
+

WEMA AUZA GARI LA DIAMOND

Lile gari jipya aina ya Nissan  Murano la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ alilompa aliyekuwa mwandani wake, Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ limezua mapya ambapo baada ya kudai linamchefua sasa anadaiwa kuwa analiuza kwa kigezo kwamba hataki gundu mwaka huu mpya wa 2015.
Gari jipya aina ya Nissan  Murano la staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ alilompa aliyekuwa mwandani wake, Beautiful Onyinye, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’
KUMBE LIPO KWA DALALI
Habari za kiwango kutoka kwa mnyetishaji wetu zilidai kwamba gari hilo lipo kwa dalali wa kike maarufu ajulikanaye kwa jina moja la Tindwa kwa ajili ya kulitafutia mteja.
NI KISASI?
Ilidaiwa kwamba, Wema ameamua kufanya hivyo kwa kuwa ana kisasi na hasira kwa Diamond kwa kuwa jamaa huyo kwa sasa anadaiwa kutoka kimapenzi na staa wa Uganda, Zarinah Hassani ‘Zari au The Boss Lady’.
“Watu wanadhani Wema anafurahishwa na Diamond kutupia mapicha na Zari baada ya kuwasifia juzikati.
“Ukweli ni kwamba hivi sasa Wema anakereka sana na jinsi Diamond anavyoweka mapicha yake na Zari wakiwa sehemu mbalimbali na anaona kuwa na gari ambalo  amepewa zawadi na Diamond ni kujipa kero zisizokuwa na sababu hivyo ameamua kuliuza,” kilisema chanzo hicho.
Aliyekuwa mwandani wa Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
HALIJAPATA MTEJA
Mpashaji wetu huyo alizidi kunyetisha kwamba pamoja na gari hilo kuwa sasa bado liko sokoni lakini halijapatia mteja wa kulinunua kitu ambacho kinazidi kumkera Madam.
“Bado gari halijapata mteja ‘so’ kitendo hicho kinamkera sana  Wema kutokana na gari hilo kutouzika mapema kwa maana kila anapoliona hajisikii vizuri kabisa,” kilisema chanzo hicho kwa sharti la kutotajwa gazeti kwani ni ‘besti’ mkubwa wa Wema.
WEMA ANASEMAJE?
Baada ya kupewa ubuyu huo, gazeti hili lilimsaka Wema ambaye alipopatikana alidai yupo bize akiandaa shoo zake za mkoani Dodoma na Morogoro.
“Ngojeni kwanza nimalize shoo zangu za mikoani. Kwa sasa nipo Dodoma nikimaliza naenda Morogoro,” alisema Wema kwa ahadi kuwa atafafanua suala hilo vizuri akitulia.
‘Diamond Platnumz’ akiwa na aliyekuwa mwandani wake Wema Isaac Sepetu ‘Madam’.
TUMEFIKAJE HAPA
Diamond alimzawadia Wema gari hilo lenye thamani ya Sh. milioni 36,  siku ya bethidei ya mwanadada huyo iliyofanyika Septemba 28, mwaka jana.
Siku chache baadaye Wema alidai kummwaga jamaa huyo huku akieleza kwamba hapendi kuliona wala kulitumia gari hilo kwani lilikuwa likimzidishia chuki juu ya jamaa huyo.
+

Friday 2 January 2015

JOKATE: DIAMOND HANA AKILI TIMAMU

Staa wa urembo, muziki, filamu na ujasiriamali Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ au ‘Jojo’ amemrushia maneno makali aliyewahi kuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuwa hana akili timamu kufuatia maneno aliyotoa kuwa enzi za uhusiano wao, eti mwanadada huyo alikuwa akichenga kumzalia mtoto.
Staa wa urembo, muziki, filamu na ujasiriamali Bongo, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ au ‘Jojo’.
MAHOJIANO
.Alisema kwamba, katika harakati zake hizo, warembo ambao alishatoka nao kimapenzi akiwemo Jokate walikuwa wakimchezea mchezo mchafu ili wasimzalie kwa kuwa alikuwa akiwaambia anahitaji mtoto kwa udi na uvumba.
MZOZO MKUBWA
Hata hivyo, madai hayo ya Diamond yalizua mzozo mkubwa kwenye mitandao ya kijamii huku warembo hao wakipigwa za uso hivyo kutafuta namna ya kujitetea.“Hao akina…(wanatajwa warembo wa Diamond) watakuwa wana matatizo ya uzazi siyo bure.
“Ndiyo maana Dangote (Diamond) ameona bora aende kwa Zari (msanii wa Uganda, Zarinah Hassan) ambaye tayari ana mwanga wa kuzaa (ana watoto watatu),” ilisomeka sehemu ya maoni juu ya madai hayo ya Diamond kwenye Mtandao wa Instagram.
Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ akiwa na Diamond.
SIKIA MADAI YA DIAMOND
Diamond alifunguka: “Jokate na Wema (Sepetu) nilitamani sana wanizalie lakini walikuwa wakichengachenga, mambo mengine ujue si ya kuzungumza lakini inauma.”
JOKATE AJIBU MAPIGO
Kufuatia tuhuma hizo nzito huku kukiwa na madai pia, kwamba Jokate aliwahi kupigwa mimba ‘akaipanchi’, mwanadada huyo alipotafutwa na mwandishi wetu kujibu ‘shitaka’ linalomkabili alianza kwa kumshangaa staa huyo wa Ngoma ya Ntampata Wapi inayokimbiza kwa sasa.
Jokate alisema anamshangaa Diamond kuyazungumza maneno hayo hadharani na inaonesha asivyokuwa na akili timamu au ambayo haijakomaa.
JOJO ASHUKA NA MISTARI
“Diamond atuache, kila siku anatuzungumzia, hana akili timamu.
“Inadhihirisha kweli hana akili kwa kuwa mtu mwenye akili zake timamu hawezi kwenda kwenye chombo cha habari na kueleza hayo aliyoyasema,” alisema Jokate akionesha kukasirishwa na maneno ya Diamond.
Wema akiwa na Diamond.
WEMA HATAKI MALUMBANO
Ukiacha Jokate na Wema ambaye naye aliwekwa kwenye kapu moja la kuchenga kumzalia, hakutaka kumjibu Diamond kwa kuwa hataki malumbano au makuu na mtu.
PENNY ALISHAJIBU
Pia jamaa huyo alimzungumzia aliyekuwa mwandani wake mwingine, Penniel Mwingilwa ‘Penny’ kuwa yeye alitoa mimba zake mbili kwa visingio tofauti.Katika majibu yake kupitia gazeti tumbo moja na hili, Risasi Jumamosi, toleo la wiki iliyopita, Penny alisema kuwa Diamond awe mkweli na aseme tatizo lake kwani anavyojua yeye hana uwezo wa kumpa mwanamke mimba.
NENO LA MHARIRI
Baada ya kila mmoja kupata nafasi ya kufunguka kivyake, ni vyema sasa malumbano yakaisha na kuuanza mwaka 2015 kwa kuchapa kazi ili kujiletea maendeleo binafsi na taifa kwa jumla.
+

WASTARA ASOMA DUA KUMUENZI SAJUKI


Msanii Wastara akiwa kainama kwenye kaburi la marehemu mumewe sajuki
Dua ya kumuombea marehemu sajuki ikiendelea.
Ndugu na jamaa wakiwa kwenye dua.
Wastara akiwa na nisha.
STAA wa filamu Bongo Wastara Juma leo amesoma dua  maalumu kama ishara ya kumkumbuka na kumuenzi aliyekuwa mume wake kipenzi , marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’.
Marehemu Sajuki alifariki dunia Januari 2.2013 , ambapo leo ametimiza miaka  miwili, dua ya kumuombea ilianzia katika makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam ambapo marehemu Sajuki alizikwa na baadae kuhamia nyumbani kwake Tabata.
Akizungumza Wastara alisema anajisikia faraja sana kusoma dua kwa ajili ya mtu aliyempenda lakini pia anawashukuru wadau na  wote waliojitokeza katika kufanikisha  kisomo hicho.
Aidha wasanii mbalimbali wamejitokeza akiwemo Mohamed Mwikonge ‘’Frank’ Mtitu, Nisha, Bond na wengineo ambao pia wameomba na kuwakumbusha wasanii na wadau mbalimbali kuwakumbuka na kuwaenzi wasanii pindi wanapoaga dunia.
+

Wednesday 31 December 2014

MILLEN MAGESE AMSAPRAIZ JOKATE

Mwanamitindo maarufu Bongo, ambaye anafanya kazi zake nje ya nchi Happyness Magesse ‘Millen’. Mwanamitindo maarufu Bongo, ambaye anafanya kazi zake nje ya nchi Happyness Magesse ‘Millen’ ambaye pia alishawahi kunyakua taji la Miss Tanzania 2001, ‘amemsapraiz’ mwanamitindo na mbunifu Jokate Mwegelo, kwa kumpatia keki yenye sura ya mdomo wake.
Awali, kulikuwa na kikao cha kawaida cha kujadili mambo mbalimbali ya kikazi baina yao kilichofanyika ndani ya hoteli ya Hyatt Kempisky, iliyopo Posta Jijini Dar, lakini kumbe Millen alikuwa ameandaa keki.
Mwanamitindo na mbunifu Jokate Mwegelo.
“Yaani mimi nilijua tunakutana kama tulivyopanga, lakini cha kushangaza nikakuta watu wakiongozwa na dada yangu Millen wameniandalia keki mbalimbali ikiwemo moja kama mdomo wangu kabisa na kidoti juu, kwa kweli nilifurahi sana siwezi kuelezea,” alisema Jokate.  
+

Tuesday 30 December 2014

DIAMOND PLATNUMZ ATUA RWANDA KWA SHANGWE


Staa wa Bongo Fleva, Naseeb Abdul 'Diamond Platnumz' akiwa na mfanyabiashara mrembo na muimbaji wa Uganda, Zarinah Hassan 'Zari'  au 'The Boss Lady' baada ya kuwasili Rwanda jana.
Diamond Platnumz (katikati) akiwa kamshika mkono mpenzi wake wa sasa Zarinah Hassan 'Zari'  au 'The Boss Lady baada ya kuwasili uwanja wa ndege wa Rwanda.
Diamond na The Boss Lady wakifanya yao.
Diamond (kulia) akiongea na wanahabari baada ya kuwasili Rwanda.
Wanahabari wakifanya yao.
+

VANESSA AWATOA KIMASOMASO WASANII WA KIKE


Vanessa Mdee.

MWANADADA anayefanya vizuri katika muziki wa Bongo Fleva, Vanessa Mdee kwa mara ya kwanza amewatoa kimasomaso wasanii wa kike Bongo kwa kutwaa tuzo ya kimataifa za All Africa Music Awards ‘AFRIMA’ nchini Nigeria.
Akizungumza na paparazi wetu Vanessa ambaye amepata tuzo ya Msanii Bora wa Kike Afrika Mashariki alisema anawashukuru mashabiki kwa kuwa wameonesha moyo wa kumpigia kura mpaka kuwashinda wasanii wengine wa Uganda na Kenya kama vile, Wahu, Size 8, Kaz (wa Kenya) na Jackie Chandiru wa Uganda.
“Nina furaha sana kwani ni mara yangu ya kwanza kupata tuzo ya kimataifa pia nimewatoa kimasomaso wasanii wenzangu wa kike, kikubwa nawashukuru mashabiki wangu kwa kunipa sapoti kubwa ya kunipigia kura, ninawaahidi kwamba nitaendelea kufanya muziki mzuri ambao wataupenda na kuwa mwanamuziki wa kimataifa zaidi,” alisema Vanessa.
Tuzo hizo zilizotolewa usiku wa Desemba 27 huko Lagos, Nigeria pia msanii Nasibu Abdul ‘Diamond’ alipata tuzo katika kipengele cha Msanii Bora wa Kiume Afrika Mashariki huku msanii Peter Msechu ambaye naye alikuwa kwenye kinyang’anyiro hicho akikosa.
+

Monday 29 December 2014

WEMA AMTAMBULISHA MSANII MPYA WA KAMPUNI YAKE


Wema Sepetu, akiwashukuru mashabiki zake kwa sapoti waliyompa kwa mwaka 2014 na kumtambulisha msanii Luna.
Msanii wa Bongo Fleva, Ally Luna (kushoto), akiimba wimbo wa kumsifia Wema mara baada ya kutambulishwa kuwa chini ya Kampuni ya Endless Fame.
Wema Sepetu akimtunza Luna.
Bob Junior akikamua jukwaani.
Msanii wa Bongo Fleva, Linex, akiimba huku shabiki yake akizungusha nyonga baada ya kuguswa na moja ya nyimbo zake.
Barnaba Boy akitumbuiza.
Mmoja wa mashabiki waliohudhuria ndani ya Club 71 akicheza na Barnaba Boy.
Mwigizaji wa filamu za Bongo, Aunt Ezekiel, akizama ndani ya Club 71 na  marafiki zake.
Msanii aliye chini ya Kampuni ya Endless Fame, Mirra, akikamua.
Mmoja wa mabaunsa wa ukumbi huo akimuondoa jukwaani mrembo mmoja baada ya kuguswa na wimbo wa Mirra na kuamua kulivamia jukwaa.

Msanii wa Hip Hop, Izzo Business, akipagawisha mashabiki.
Godzilah akitoa burudani.
Mtangazaji wa Clouds FM, Soud Brown, akiwa na  keki aliyopewa na Wema Sepetu kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa ambayo ilifanyika usiku huo.
Soud Brown akimlisha kipande cha keki Wema Sepetu.
Mmoja wa mapaparazi wa mtandao huu Musa Mateja (kulia), akilishwa keki na Soud Brown.
Msanii wa Bongo Movie, Aunt Ezekiel, akilishwa keki.
Wema akiselebuka na meneja wake Martine Kadinda.
MKURUGENZI wa kampuni ya Endless Fame, Wema Sepetu,  usiku wa kuamkia leo amemtambulisha msanii mpya wa Bongo Fleva, Ally Luna, ambaye takuwa mmoja wa wasanii wa kampuni hiyo na kusimamiwa shughuli zote za kimuziki kama ilivyo kwa mwanamuziki Mirra.
Tukio hili lilifanyika ndani ya Ukumbi wa Club 71 uliopo Tegeta jijini Dar es Salaam ambapo kulikuwa pia na shoo maalum ya  kufunga mwaka kwa kampuni hiyo na kuwashukuru wadau wote waliowaunga mkono.
Shoo hiyo ilisindikizwa na wasanii kibao wa Bongo Fleva, wakiwemo Bob Junior, Godzilah, Izzo Business, Barnaba Boy, Linex na Mirra.
+