Monday 29 December 2014

Leave a Comment

WEMA AMTAMBULISHA MSANII MPYA WA KAMPUNI YAKE


Wema Sepetu, akiwashukuru mashabiki zake kwa sapoti waliyompa kwa mwaka 2014 na kumtambulisha msanii Luna.
Msanii wa Bongo Fleva, Ally Luna (kushoto), akiimba wimbo wa kumsifia Wema mara baada ya kutambulishwa kuwa chini ya Kampuni ya Endless Fame.
Wema Sepetu akimtunza Luna.
Bob Junior akikamua jukwaani.
Msanii wa Bongo Fleva, Linex, akiimba huku shabiki yake akizungusha nyonga baada ya kuguswa na moja ya nyimbo zake.
Barnaba Boy akitumbuiza.
Mmoja wa mashabiki waliohudhuria ndani ya Club 71 akicheza na Barnaba Boy.
Mwigizaji wa filamu za Bongo, Aunt Ezekiel, akizama ndani ya Club 71 na  marafiki zake.
Msanii aliye chini ya Kampuni ya Endless Fame, Mirra, akikamua.
Mmoja wa mabaunsa wa ukumbi huo akimuondoa jukwaani mrembo mmoja baada ya kuguswa na wimbo wa Mirra na kuamua kulivamia jukwaa.

Msanii wa Hip Hop, Izzo Business, akipagawisha mashabiki.
Godzilah akitoa burudani.
Mtangazaji wa Clouds FM, Soud Brown, akiwa na  keki aliyopewa na Wema Sepetu kama zawadi ya siku yake ya kuzaliwa ambayo ilifanyika usiku huo.
Soud Brown akimlisha kipande cha keki Wema Sepetu.
Mmoja wa mapaparazi wa mtandao huu Musa Mateja (kulia), akilishwa keki na Soud Brown.
Msanii wa Bongo Movie, Aunt Ezekiel, akilishwa keki.
Wema akiselebuka na meneja wake Martine Kadinda.
MKURUGENZI wa kampuni ya Endless Fame, Wema Sepetu,  usiku wa kuamkia leo amemtambulisha msanii mpya wa Bongo Fleva, Ally Luna, ambaye takuwa mmoja wa wasanii wa kampuni hiyo na kusimamiwa shughuli zote za kimuziki kama ilivyo kwa mwanamuziki Mirra.
Tukio hili lilifanyika ndani ya Ukumbi wa Club 71 uliopo Tegeta jijini Dar es Salaam ambapo kulikuwa pia na shoo maalum ya  kufunga mwaka kwa kampuni hiyo na kuwashukuru wadau wote waliowaunga mkono.
Shoo hiyo ilisindikizwa na wasanii kibao wa Bongo Fleva, wakiwemo Bob Junior, Godzilah, Izzo Business, Barnaba Boy, Linex na Mirra.

0 comments: