Friday 2 January 2015

Leave a Comment

WASTARA ASOMA DUA KUMUENZI SAJUKI


Msanii Wastara akiwa kainama kwenye kaburi la marehemu mumewe sajuki
Dua ya kumuombea marehemu sajuki ikiendelea.
Ndugu na jamaa wakiwa kwenye dua.
Wastara akiwa na nisha.
STAA wa filamu Bongo Wastara Juma leo amesoma dua  maalumu kama ishara ya kumkumbuka na kumuenzi aliyekuwa mume wake kipenzi , marehemu Juma Kilowoko ‘Sajuki’.
Marehemu Sajuki alifariki dunia Januari 2.2013 , ambapo leo ametimiza miaka  miwili, dua ya kumuombea ilianzia katika makaburi ya Kisutu, jijini Dar es Salaam ambapo marehemu Sajuki alizikwa na baadae kuhamia nyumbani kwake Tabata.
Akizungumza Wastara alisema anajisikia faraja sana kusoma dua kwa ajili ya mtu aliyempenda lakini pia anawashukuru wadau na  wote waliojitokeza katika kufanikisha  kisomo hicho.
Aidha wasanii mbalimbali wamejitokeza akiwemo Mohamed Mwikonge ‘’Frank’ Mtitu, Nisha, Bond na wengineo ambao pia wameomba na kuwakumbusha wasanii na wadau mbalimbali kuwakumbuka na kuwaenzi wasanii pindi wanapoaga dunia.

0 comments: