Wednesday 17 December 2014

Leave a Comment

JINSI YA KUGUNDUA MAAMBUKIZI KWENYE UZAZI (DIAGNOSIS OF PID)

Baadhi ya wagonjwa watahitajika kulazwa hospitali ambapo watapewa dawa za saa na kuwa chini ya uangalizi wa haraka wa manesi na madaktari.Wagonjwa wanaohitaji kulazwa ni kama wale wanaodhaniwa kuwa wana uvimbe au jipu kwenye mfuko wa mayai yaani tube ovarian abscess au wale wenye kutapika sana na wenye homa kali pia wenye maumivu makali ya tumbo yanayofanana na kidole tumbo. Wagonjwa ambao hawakupata nafuu baada ya matumizi ya dawa ya awali baada ya saa 48 ya kumaliza dawa na wale walioshindwa kumeza dawa pia wagonjwa wenye rirusi vya ukimwi watahitajika kulazwa.
Dawa zinazotumika kwa wale waliolazwa ni kama vile cefoxitin na clindamycine ikichanganywa na gentamycine.Nafuu ya mgonjwa itajulikana baada ya mgonjwa kujisikia vizuri na homa itashuka,  pia maumivu ya tumbo yatapoa na vipimo vya maabara vitaonyesha kuwa vijidudu vimeisha.
Baadhi ya wagonjwa watahitaji upasuaji kama kutakuwa na madhara makubwa (complications) kama vile vijidudu kuingia kwenye utumbo, jipu kwenye viungo vya uzazi (pelvic abscess) usaha kwenye mfuko wa mayai (turbo ovarian abscess).
JINSI YA KUJIKINGA (PREVENTION)
Kwanza, matabibu wana wajibu wa kuelimisha jamii juu ya maambukizi yanavyotokea na kujiepusha nayo.
Pili, jamii iepushwe mwanamke kuwa na uhusiano wa kingono na wanaume wengi (multiple sexual partiners) na watu wajue matumizi sahihi ya kondom.
Mwanamke lazima amlete mwenza wake ili aweze kufanyiwa vipimo vya uhakika na akithibitika hana maambukizi ya kisonono basi ataweza kupewa dawa za kuua vijidudu vya clamydia maana ni vigumu kuweza kugundua vijidudu vya clamydia. Mwenza wake yaani atumie dawa kwa muda wa siku saba.
Ufuatiliaji wa mgonjwa kwa kumpima  ufanyike baada ya wiki moja baada ya wote kutibiwa.
Kwa mwanamke apimwe kila anapomaliza hedhi na majibu yaonyeshe kuwa hana ugonjwa, upimaji ufanyike mara tatu mfululizo na majibu yaonyeshe kuwa hana ugonjwa. Mtu yeyote atakayejihisi ana tatizo hili asitumie dawa hizo bila kuonana na daktari ambaye atampima.

0 comments: