
MTANGAZAJI 
 wa Redio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amesema siku zote anapokuwa 
kwenye uhusiano wa kimapenzi akigundua mtu wake ana ‘date’ na mwanamke 
mwingine, kamwe hatathubutu kugombea bwana ila atanawa mikono.
Mtangazaji wa Redio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ akipozi.
Akiongea hivi karibuni Dida alisema, hakuna kitu 
ambacho kwake anaona ni cha kipuuzi kama kugombea penzi, kwa kuwa mtu 
anapokusaliti ni wazi upendo wake umehamia kwa mtu mwingine hivyo hawezi
 kujing’ang’aniza.
Mtangazaji wa Redio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ akipozi.“Nawashangaa sana wasichana wanaokosa kazi ya kufanya kwa kuanza kuwagombea wanaume, wengine wanadundana hadi kutoana manundu, hivi nigombee bwana kwani wanaume wameisha? Mimi nikimkuta mtu wangu yupo na mtu mwingine wala sijishughulishi, nachukua hamsini zangu,” alisema Dida.




0 comments:
Post a Comment