Wednesday 17 December 2014

Leave a Comment

Catherine Samba-Panza: ‘Kigogo’ aliyemaliza maafa Afrika ya Kati


 
.


Watu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati na Jumuiya ya Kimataifa haitasahau namna mwama mama Catherine Samba alivyorejesha amani na mshikamano katika nchi hiyo.
Catherine aliyekuwa Meya wa Jiji la Bangui kuanzia Mei mwaka 2013, alipata nafasi ya pekee ya kupendekezwa kushika wadhifa wa urais wa mpito miezi minane baadaye na kisha kuapishwa Januari 23, 2014 siku 12 tangu kuachia ngazi wa Dtojidia.
Catherine aliyezaliwa Juni 26, 1954 alivunja rekodi na kuweka historia kwa kuwa rais wa kwanza wa mpito kwa miezi 18 ambayo bado anaitumikia, lakini pia kuwa rais wa kwanza mwanamke katika taifa hilo lililokuwa likipitia kipindi cha mpito kutokana na machafuko makali.
Aliteuliwa kuwa Meya wa Jiji la Bangui, mji Mkuu wa CAR chini ya Baraza la Mpito la Taifa (CNT) baada ya mgogoro uliolikabili taifa hilo kwa karibu mwaka mmoja, kuanzia mwaka 2012.
Uteuzi wake ulikubaliwa na pande zote mbili ziliziokuwa zikipingana, upande wa Seleka na Anti-balaca.
Katika uteuzi huo, Catherine ambaye alikuwa mwanasheria na mfanyabiashara kabla ya kuingia katika siasa alikubalika pia na Rais Francois Hollande wa Ufaransa, ambaye alikuwa akitafuta namna ya kumaliza mgogoro wa taifa hilo.
Hata hivyo, awali hakutarajiwa kupata nafasi hiyo ya kuwa rais wa mpito, kwa kuwa kulikuwa na zaidi ya watu wanane waliokuwa wakitajwa kufikiriwa kupewa nafasi hiyo, lakini walitakiwa kuthibitisha kwamba hawana uhusiano na makundi hayo mawili, yaani Seleka na Anti-balaka.
Suala la kwanza, mama huyo anaweka historia na kuwa mwanamke wa kwanza kushika wadhifa huo na zaidi kwa kufanikiwa kurejesha amani na utulivu kuelekea kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwakani.
Hotuba yake aliyoitoa kwa ujasiri baada ya kuthibitishwa na bunge la nchi hiyo akiwataka wahusika kuweka chini zana zao na kusitisha mapigano ilikuwa na matunda makubwa.
Hakusita kuugeukia upande wa pili wa Seleca ambao kwa kuwa walikuwa ndio waathirika wakubwa, aliwataka waache woga na kwamba hakuwa tayari kusikia tena mauaji ya watu wasio na hatia, kwa kujipambanua kwamba ni rais wa watu wote bila kuwa na ubaguzi.
Wito wake wa kutaka mazungumzo baina ya pande mbili zilizohusika kwenye mgogoro wa kisiasa uliitikiwa kikamilifu na pande zote mbili, na japokuwa aliingia madarakani katika kipindi ambacho hakikuwa na utawala wa sheria, aliweza kurejesha taifa hilo kwenye mstari na kuepuka kile kilichohofiwa kutokea, mauaji makubwa ya kimbari kama ilivyowahi kutokea Rwanda.
Chanzo cha machafuko
Machafuko katika nchi hiyo yalishika kasi baada ya Rais Michael Dtojodia kupindua Serikali na kuchukua madaraka.
Hatua hiyo ilivuruga amani ya taifa hilo na kuibua mapambano baina ya makundi mawili yaliyokuwa na mitizamo ya kidini, Seleka na Anti-Balaka kuingia katika machafuko yaliyolielekeza taifa hilo kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe.
Baada ya Djotodia aliyeingia madarakani Machi 24, 2013 kwa kumuondoa Rais Francois Bozize, kukubali kuachia madaraka Januari 10 mwaka huu kutokana na shinikizo kali la ndani na Jumuiya ya Kimataifa, alitoa nafasi ya kuibuka kwa mwanamama Catherine.

0 comments: